Shamba la Wananchi lililoko
katika wilaya ya Mbarali katika kata ya Kapunga ambalo limekuwa liktumia
maji kwa muda wote bila ya kuyalipia chochote Serikalini lijulikanalo kama
Mwashikamile lenye ukubwa wa ekari 800 limepewa ruhusa ya kufungua mfereji wa
maji uliokuwa umefungwa baada ya Shamba hilo kulipa madeni yote ya maji na
kulipa faini waliyopigwa na Kikosi kazi cha Kitaifa cha kunusuru Mto Ruaha.
Akiongea na Wananchi wa eneo hilo la mwashikamile Mwenyekiti wa Kikosi
kazi hiko Bwana Richard Muyungi amewahimiza viongozi wa shamba hilo kuhakikisha
hawaenedelei kuchepush mifereji ya maji bila kuyalipia na kutekeleza maagizo ya
serikali ya kupata vibali vote halal vya matumizi ya maji na kilimo cha
umwagilaji. Kikosi kazi kimewaruhusu Wananchi kuendelea na umwagiliaji wa maji
katika mashamba yao ya Mpunga mpaka pale watakapovuna.
Bwana Muyungi alisisitiza kuwa
hakuna wananchi wote wameruhusiwa kuendelea kutumia maji hadi kuhakikisha kuwa
mazao yote mashambani yanavunwa la msingi ni kuea maji hayo wayalipie. Alsema
wananchi katika mashamba memgi tayari wamekwishatoa michango ya kulipia maji
lakini viongozi hawataki kulipia maji jambo ambalo haliwezi kuvumilika. Aidha
akiongea, Mwenyekiti wa eneo hilo la Mwashikamile Bwana Leonard
Mwashikamile ameshukuru sana Kikosi kazi kwa kuwaruhusu tena kufungua
mfereji wa maji na pia aliahidi kwa niaba ya Wananchi wa kijiji hicho kutunza
maji yote yanayotumika kwa umwagiliaji
na kuwa atahakikisha Wananchi hawachepushi maji ya wizi tena.
Shamba la Mwashikamile
lilikuwa ni moja kati ya mashamba pamoja na skimu za umwagiliaji
zilizopigwa faini na Kikosi kazi cha Kitaifa cha kunusuru ikolojia ya Mto Ruaha
katokana na kuchepusha maji bila kuyalipia na bila kibali chochote..
No comments:
Post a Comment