WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kusimamia biashara ya mazao mbalimbali katika maeneo yao ili wakulima waweze kupata tija.
Pia
amesema Bodi ya Mazao Mchanganyiko inazunguka nchi nzima kupata taarifa
za bei ya mazao hayo ili kujirisha iwapo wanunuzi wa mazao mchanganyiko
ya wakulima kama wananunua kwa bei inayostahili.
Alitoa
agizo hayo jana (Alhamisi, Julai 20, 2017) wakati akizungumza na
wananchi wa kijiji cha Ilasilo kilichoko katika mpaka wa mkoa wa Mbeya
na Songwe alipokuwa njiani kuelekea wilayani Songwe kwa ajili ya ziara
ya kikazi.
Alisema
kwa sasa bodi hiyo inazunguna nchini kote kutafuta taarifa za bei za
mazao ili kubaini bei zinazotumiwa na wanunuzi wa mazao hayo kama
zinastahili baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wakulima wa eneo
hilo.
“Wakulima
msikubali kuuza mazao ovyo, wekeni na akiba ya chakula. Pia Bodi ya
Mazao Mchanganyiko itakuja hapa kwa kuwa sasa inapita sehemu mbalimbali
kupata taarifa za bei za mazao pamoja na kuwatafutia masoko yenye tija.”
Pia
Waziri Mkuu aliwaagiza watu wote wanaohusika na suala la usambazaji wa
pembejeo kuhakikisha wanazifikisha kwa wakulima katika kipindi
kisichopungua muda wa miezi miwili kabla ya kuanza kwa msimu ili
kuwaondolea changamoto ya uchelewashwaji wa huduma hiyo
Kwa
upande wake Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Bi. Chiku Gallawa alitaja
changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya kilimo ni kutokuwepo kwa
soko la uhakika la mazao pamoja na uingizwaji wa pembejeo zisizofaa
katika mkoa.
Alisema
tayari mkoa umechukua hatua mbalimbali za kukabiliana na changamoto
hizo kwa kuhimiza matumizi ya teknolojia ya kisasa kama matumizi ya
mbegu bora zinazostahimili hali ya hewa iliyopo na zinazokomaa kwa muda
mfupi.
Pia
wataalamu wa kilimo walichunguza pembejeo zinazotumika katika mkoa huo
ambapo walibaini asilimia 60 ya viuatilifu na asilimia 20 hadi 30 ya
mbegu zinazouzwa madukani na kutumiwa na wakulima katika wilaya za Momba
na Mbozi ni bandia.
Alisema
matokeo ya kutumia pembejeo hizo yalisababisha mavuno ya mahidi
kupungua kutoka magunia 25 hadi magunia manane kwenye ekari moja katika
msimu wa kilimo wa mwaka 2012/2013.
Mkuu
huyo wa Mkoa alitaja mikakati waliyojiwekea katika kukabiliana na
changamoto hiyo kuwa ni kufanya ukaguzi kwenye maduka yote yanayouza
pembejea pamoja na kutoa elimu ya kutambua pembejeo zisizifaa ili watoe
taarifa mapema na wahusika wachukuliwe hatua.
No comments:
Post a Comment