Social Icons

Wednesday, August 16, 2017

MOTO MKUBWA WATEKETEZA SOKO LA SIDO USIKU HUU JIJINI MBEYA

Moto huo ukiendelea kuteketeza bidhaa mbalimbali zilizomo sokoni humo.
Moto huo ukiendelea kuteketeza bidhaa mbalimbali zilizoachwa sokoni hapo, huku Kikosi cha Zima Moto kikiendelea kupambana nao.
Moto huo ukiendelea kuteketeza bidhaa mbalimbali zilizoachwa sokoni hapo
 
Taarifa zilizotufikia hivi punde kutoka kwa Ripota wetu jijini Mbeya,zinaeleza kuwa Soko la Sido lililopo mkabala na maeneo ya Mwanjelwa linateketea kwa moto hivi sasa,Taarifa zinaeleza kuwa chanzo cha moto huo bado hakijajulikana mpaka sasa.
Kwa mujibu wa Ripota wetu aliyepo eneo la tukio, moto huo ulianza kuwaka mnamo majira ya saa tatu usiku na kusababisha tafrani kubwa kwa  watu waliokuwepo maeneo hayo, ambao nao walionesha juhudi zao za kushriki kuuzima, kwa bahati nzuri kikosi cha zima moto kikawasili na kupambana na moto huo uliokuwa ukiwaka kwa kasi kubwa.
Katika kuongeza nguvu za usalama eneo hilo, kikosi kutoka Jeshi la Polisi la mjini Mbeya liliwasili katika eneo hilo katika  kuhakikisha ulinzi na usalama wa mali za watu unaimarika .
TAARIFA ZAIDI TUTAWALETEA
 

No comments:

Post a Comment