Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura
akikagua uwanja wa Machinga uliopo mjini Tukuyu ambao umebadilishwa
matumizi na Halmashauri ya Rungwe kwa kukosa sifa w badala yake uwanja
wa michezo sasa utakuwa unatumika ule wa Tandale mjini humo.
Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura
akiongea na wananchi na wanamichezo (hawapo pichani) waliokuwa
wanashiriki Tamasha la Ngoma za Jadi linaloratibiwa na Taasisis ya Tulia
Trust mjini Tukuyu
Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura
(wa pili kushoto) na Naibu Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt. Tulia Ackson wakibeba nyoka anyetumiwa kwa kucheza ngoma ya
Bogobogobo kutoka Bujora Mwanza.
(Picha na Eleuteri Mangi, WHUSM, Tukuyu)
………………………………………………………………………………
Na Eleuteri Mangi, Tukuyu, Mbeya.
Halmashauri
ya Rungwe imebadilisha matumizi ya uwanja wa zamani wa mpira wa miguu
uliopo mjini Tukuyu unaojulikana kama machinga kuendelea kutumika kwa
matumizi mengine kutokana na kukosa sifa za uwanja huo kukosa sifa.
Badala
yake Halmashauri hiyo imetoa uwanja wa Tandale uliopo mjini Tukuyu
kutumika kwa michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu na matamasha
mbalimbali.
Hayo
yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Tukuyu Bw. Julius Chalya alipokuwa
akitoa taarifa fupi ya shughuli za maendeleo katika wilaya hiyo kwa
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura
alipokuwa katika ziara ya kikazi mkoani Mbeya.
“Uwanja
wa mwanzo unaojulikana kama uwanja wa Machinga uliokuwa unatumika kwa
michezo kwa sasa haufai kwa matumizi ya michezo kwa kukosa sifa, hivyo
halmashauri imebadilisha matumizi yake ili uendelee kutumika kwa
matumizi mengine ikiwemo kituo cha mabasi yanayotoa huduma katika
halmashauri na bishashara nyingine” alisema Mkuu huyo wa Wilaya.
Akizungumzia
kuhusu uamuzi wa halmashauri wa kubadilisha matumizi ya uwanja huo
wakati wa kufunga Tamasha la pili la Ngoma za Asili linaloendeshwa na
Taasisi ya Tulia Trust, Naibu Waziri Wambura amesema kuwa Serikali
inaendelea kusisitiza halmashauri ziendelee kutenga maeneo yanayofaa kwa
michezo kwa kutimiza vigezo vinavyotakiwa kwa ajili ya michezo.
Uwanja
wa Tukuyu uliokuwa unatumika zamani kwa michezo umekosa vigezo vya
kuendelea kutumika kama uwanja wa michezo kutokana na vipimo vyake
kuonesha kuwa ni mdogo kwa kiwango cha halisi unatakiwa kuwa na urefu wa
mita 68 na huo wa Tukuyu una mita 44.
Kuhusu
kuendeleza kiwanja cha Tandale ambao umetolewa na halmashauri kwa ajili
ya michezo, Naibu Waziri Wambura ameliagiza Baraza la Michezo la Taifa
(BMT) kupitia Katibu Mtendaji wake Mohamed Kiganja kushirikiana na
halmashauri hiyo kwa kutoa ushauri wa kitaalamu kuendeleza uwanja huo
ili wananchi wa Rungwe waweze kuutumia kuboresha afya zao kwa kufanya
mazoezi pamoja kunufaika na fursa za kiuchumi wakati wa mashindano
mbalilmbali yatakayofanyika uwanjani hapo.
Kupatikana
kwa uwanja wa Tandale utnaotumika kwa sasa kwa michezo mbalimbali mjini
Tukuyu kumepokelwa na kwa furaha na wananchi waliofurika viwanja hivyo
wakati wa kuhitimisha Tamamsha la pili la Ngoma za Jadi linaloratibiwa
na Taasisi ya Tulia Trust ambapo mwasisi wake Naibu Spika wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania ameanza kampeni ya kuirudisha timu ya Tukuyu Stars
kwa kuwahamasisha Wabunge wa mkoa wa Mbeya na wananchi kuiwezesha timu
hiyo kurudi Ligi Kuu ya Tanzania ya Vodacom.
No comments:
Post a Comment