Hakimu
Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Michael Mteite
amekataa kujitoa kusikiliza kesi inayomkabili mbunge wa Mbeya Mjini,
Joseph Mbilinyi maarufu Sugu na mwenzake.
Sugu
na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga
wanashtakiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John
Magufuli wanayodaiwa kuitoa Desemba 30,2017.
Awali,
leo Alhamisi Januari 25,2018 Sugu na Masonga waliwasilisha ombi
mahakamani wakimkataa hakimu huyo wakitaka ajitoe kusikiliza kesi kwa
maelezo kuwa hawana imani naye.
Hakimu Mteite amesema sababu zilizotolewa na akina Sugu hazipo kisheria na hazimfanyi kujitoa.
Baada
ya hakimu kukataa kujitoa, mawakili Boniface Mwabukusi, Hekima Mwasipu
na Sabina Yongo wanaowawakilisha washtakiwa walitangaza kujitoa katika
shauri hilo.
Sugu na Masonga wameiomba Mahakama kuwapatia wiki mbili za kutafuta mawakili wengine.
Hakimu Mteite ameahirisha kesi hadi Februari 2,2018 na ameamuru washtakiwa kurejeshwa rumande.
Chanzo: Mwananchi
No comments:
Post a Comment