Mahakama
ya Hakimu Mkazi Mbeya imewatia hatiani mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph
Mbilinyi maarufu Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu
Kusini, Emmanuel Masonga na kuwahukumu kifungo cha miezi mitano jela.
Hukumu hiyo imetolewa leo Februari 26,2018 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Michael Mteite.
Sugu na Masonga wamehukumiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.
Wawili
hao wanadaiwa kutenda kosa hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika
Desemba 30,2017 eneo la Uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.
No comments:
Post a Comment