Social Icons

Thursday, July 27, 2017

JUBILEE INSURANCE YAADHIMISHA MIAKA 80 KWA KUJENGA VYOO SHULE YA MSINGI ITIJI JIJINI MBEYA


 Jubilee Insurance katika kuadhimisha miaka 80 ya kuanzishwa kwa kampuni hiyo ya bima imezinduwa vyoo katika shule ya  msingi Itiji iliyopo jijini Mbeya, vyoo hivyo vyenye jumla ya matundu 12 vilivyo jengwa na kampuni hiyo ya bima ya Jubilee Insurance na kuzinduliwa na  Meneja wa kanda nyanda za juu mamlaka ya bima Tanzania,  Consoleta Cabone baada ya kuguswa na changamoto ya  vyoo katika shule mbalimbali za msingi nchini.
 Meneja wa kanda nyanda za juu mamlaka ya bima Tanzania,  Consoleta Cabone akizungumza baada ya kukabidhi vyoo hivyo, ambapo alisema "Naipongeza sana Jubilee Insurance kwa kujitoa kujenge vyoo vya wanafunzi wa shule ya msingi Itiji, kwani ni jambo kubwa na linalo fanya na wacheche na badara ya kufanya sherehe kubwa katika maoteli kugawana kile kilicho baki kwenye bima na hatimae kurejeshwa kwa wananchi kwa kufanya mambo mema yenye baraka ikiwemo hili la ujenzi wa vyoo kwenye shule mbalimbali za msingi" pia Consoleta Cabone alitoa wito kwa wakazi wa maeneo hayo yanayozungukwa na shule hiyo kulinda na kudhamini vyoo vilivyo jengwa na Jubilee Insurance.
Meneja wa Tawi la  Jubilee Insurance kwa nyanda za juu kusini, Anne Qares akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi Meneja wa kanda nyanda za juu mamlaka ya bima Tanzania, Consoleta Cabone katika uzinduzi na ufunguzi wa vyoo vya wanafunzi wa shule ya msingi Itiji vyoo vilivyo jengwa na Jubilee Insurance.
 Mkuu wa Shule ya msingi Itigi Mwl Lightness E. Makundi Akitoa shukran kwa Jubilee Insurance kwa ujenzi wa vyoo vya wanafunzi katika shule yake.
  Mgeni rasmi akiwa katika zoezi  la uzinduzi wa vyoo shule ya msingi Itiji iliyopo jijini mbeya.

No comments:

Post a Comment